Matthew 12:22-24

Yesu Na Beelzebuli

(Marko 3:20-30; Luka 11:14-23)

22 aKisha wakamletea mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, na alikuwa kipofu na bubu. Yesu akamponya, hata akaweza kusema na kuona. 23 bWatu wote wakashangaa na kusema, “Je, yawezekana huyu ndiye Mwana wa Daudi?”

24 cLakini Mafarisayo waliposikia jambo hili wakasema, “Mtu huyu anatoa pepo wachafu kwa uwezo wa Beelzebuli,
Beelzebuli au Beelzebubu; pia 12:27.
mkuu wa pepo wachafu.”

Copyright information for SwhNEN